Bwana Yesu
asifiwe
Kuna siri
kubwa imejificha katika tendo la msamaha, hebu tujifunze kwa kina siri hii
huenda ikasaidia kuponya majeraha na machungu yaliyomo katika nafsi yako.
Yapo mambo
kadha tunaenda kujifunza kama yafuatayo
1. Msamaha
ni nini
2. Kwanini
tusamehe
3. Msamaha
unafaida gani/ umuhimu gani
4. Ninawezaje
kusamehe
5. Nini
matokeo ya kuto kusamehe
Msamaha
Ni tendo la
kumuachilia mtu ambaye amekusababishia maumivu katika moyo wako, Ni tendo la
kumuondolea hatia mtu ambaye amekufanyia mambo yaliyopelekea moyo wako kuumia/
kupata uchungu
Sala ya Bwana
inasema “Utusamehe makosa yetu kama sisi tuwasamehevyo wanaotukosea” Kwanini
Mungu akupe kusamehe kwanza ndo upate kusamehewa?
Msamaha ndio
unaokupa uhai pamoja na Mungu, ule uhai ndio unaokupa wewe nguvu ya kusamehe
wengine, wapo baadhi ya watu wapo tayari kufa
kuliko kusamehe watu wengine, ni ukweli
wa ajabu japo msamaha ni mchakato mgumu na mgumu. Sio jambo linalofanyika usiku
mmoja. Ni mageuzi ya moyo, ni neno ndogo
na rahisi, lakini ni ngumu sana kumsamehe mtu ukiwa umeumizwa sana.
Kumsamehe mwingine hakufuti kumbukumbu za zamani za
machungu uliyoyapata bali kunaondoa uchungu kupitia uponyaji unaotokana na
tendo hilo la msamaha. Msamaha
ndio unaokupa kibali mbele za Mungu, lazima ukubali gharama kusamehe ni gharama
tena kubwa
Yapo mambo
haya
1. Luka
17:3 “Jilindeni, kama ndugu yako akikosa mwonye akitubu msamehe”
Neno
hili linaeleza habari za kugawana
gharama, kwanza kama ndugu akikosa mwonye, pili akitubu msamehe. Upo uwezekano
wa mtu huyo kukataa kutubu Je? Asipo kubali maonyo unafanya nini hapo.
Usisubiri kuombwa msamaha ndo usamehe.
2. Warumi
5:8 “Bali Mungu aonesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwakuwa kristo
alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi”
Hii
ni hatua kubwa ya msamaha ambayo kila mtu anatakiwa kuwa nayo, kristo alikufa
kwa ajili yetu tukiwa tungali wenye dhambi, alitangaza msamaha kwetu tungali
watendaji wa mambo yaleyale ambayo ni chukizo kwake
Usisubili
kuombwa msamaha, eti hajaomba msamaha nimeshindwa kumsamehe, alitakiwa kuombe
msamaha ndo nimsamehe, kama unasubiri kuombwa msamaha ujue kuuona ufamle wa
mbinguni kwako itakuwa ngumu
Lazima
ukubali kubeba gharama zako na za yule unaye msamehe, kumuonya aliye kokosea ni
kutaka kugawana gharama ambazo ulitakiwa kuzibeba wewe mwenyewe. Ukijivika ujasili
utaweza kusamehe
Msamaha ni
tiba ya nafsi, hurejesha kila kilicho potea, huleta upatanisho, huondoa hukumu,
hurejesha mahusiano yaliyo potea
Zab 103 2-5 Akusamehe maovu yako yote,
akuponya magonjwa yako yote, aukomboa uhai wako na kaburi, akutia taji ya
fadhiri na rehema, aushibisha mema uee wako, ujana wako aurejesha kama tai.
Aliye kuumiza
hawezi kukuondolea maumivu wala uliye muumiza huwezi kumwondolea maumivu, bali
kristo mwenyewe ndani yetu ndiye awezaye kutuondolea maumivu, majeraha na
machungu iwapo tu utampa nafasi.
Tendo alilolifanya
Yesu lilikuwa la kijasiri, hata wewe unaweza kuwa jasiri kama Yesu kwakuwa hupo
ndani yako, mruhusu akusaidie kufanya maamuzi magumu.
“Nayaweza mabo yote katika yeye anitiaye
nguvu” Nguvu ya kusamehe inattegemea
maamuzi yako, Vile unavyo amua kusamehe
ndinyo Mungu anavyo kutia nguvu za kusamehe
Unacho hitaji ni kusamehe na kusahau bila kujali kafanya
nini na ni nani na kwanini ili uishi maisha furaha, kusamehe ni uwezo wa
kukubali ukweli wa mambo.
Kusahau ni kukubali, huwezi kusahau kile mtu
alichokufanyia, lakini yote unahitaji tu kufanya ni kukubali ukweli kwamba
uliopita umepita na kuondoa chuki hizo moyoni mwako.
Huna haja ya kusubiri au kusikia mtu anakuja kwako kuomba msamaha ili umsamehe.
Haiwezi kamwe kuja. Hebu msamaha uwe maisha yako “Tabia yako” ambayo haitategemea
tabia ya mtu mwingine, bali kwa moyo wako wa ukarimu.
Ebr 12:14 Tafuteni
kwa bidii kuwa na amani na watu wote na huo utakatifu ambao hakuna mtu atakaye
muona Mungu asipokuwa nao. Kila mwenye matarajio ya kwenda mbinguni ni lazima roho ya msamaha iwe maisha yake, Utaishi kwa
amani, kwa furaha, hutakuwa nauchungu kamwe.
Fuatilia
zaidi masomo mengine:-
Youtube : Mungu
anakupenda
Twitter : Mungu
anakupenda
Facebook
: Mungu anakupenda