Wakati
wa kuoa ni wakati wa ujana Mal 2:14 Biblia
inasema mke wa ujana wako, hii inaonesha kibiblia wakati sahihi wa kuoa ni wakati
wa ujana, hakuna wakati mwingine ambao ni sahihi sana wa kumpata mwenzi wa
maisha isipokuwa ujanani.
Mtu
wa kwanza kuwepo duniani ni kijana moja Adamu na mkewe Hawa ambao Mungu aliwapa
maagizo ili wazae ili tuongezeke, Kabla hawajatenda dhambi Adamu anazungumza “Utamwacha
baba yako na mama yako utaambatana na mwenzi wako na mtakuwa mwili mmoja” hata hakujawa na dhambi
duniani.
Tunapozungumza
suala la mahusiano ya kijana na Binti tunazungumzia suala takatifu kwasababu
aliyelianzisha wa tendo hili ni
mtakatifu, ni sisi tumekuja kuingiza mambo mengi na kufanya suala hili
kuharibika
Mahusiano
yanapitia hatua kadha wa kadha kama
ifuatavyo:-
1. Urafiki
Ni
mahusiano ya kawaida ambayo kijana wa kiume na kijana wa kike wanaweza kuwa
wanashirikiana katika mambo mbalimbali ya kijamii, kimasomo, kiuchumi hata
kisiasa bila kuwa na agenda nyingine
2. Uchumba
Ni
mahusiano ya kijana wa kiume na kijana wa kike ambao wamekwisha peana ahadi ya
kuoana. Katika hatua hii huwezi kumuita mchumba wako mke au mume.
Ni kipichi cha matazamio cha watu wawili wa jinsia ya kiume na jinsia ya kike kabla ya kuoana au kuna Ahadi ya kuoana, uchumba sio urafiki wala sio ndoa.
Ni kipichi cha matazamio cha watu wawili wa jinsia ya kiume na jinsia ya kike kabla ya kuoana au kuna Ahadi ya kuoana, uchumba sio urafiki wala sio ndoa.
3. Ndoa
Ni
mahusiano ya kijana wa kiune na kijana wa kike ambao wamekwisha weka agano la
kuishi kama mume na mke.
Kuna agano la watu wawili wa jinsia ya kiume na jinsia ya kike la kuishi pamoja kama mume na mke.
Kuna agano la watu wawili wa jinsia ya kiume na jinsia ya kike la kuishi pamoja kama mume na mke.
Mambo
ya kuzingatia kwa kijana wa kiume kabla hujatafuta mwenzi:-
1. Kumpokea yesu
Ukipatana
na Mungu, Mungu Mungu atakusikiliza nawe utasikiliza, Ni vema kupatana na Mungu
kwanza.
2. Kufanya kazi
Usichumbie
kama huna kazi, Mwa 2:8 Mungu alimuweka
Adamu Edeni kwanza alime (Afanye kazi) ndipo alipo mletea mke (Hawa)Mwa 2:18 hivyo lazima ufanye kazi
3. Kupata mwenzi
Mwa
2:18 Neno linasema “Bwana Mungu
akasema,Si vema mtu huyu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana nae.”
Hata
kama umewahi kukosea katika kufanya uchaguzi ikakupelekea kuumizwa bado una
nafasi ya kuinuka tena Mit 24:16 “Bali mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena;
Bali wasio haki hukwazwa na mabaya” Inawezeka na mpaka sasa
umefikia mahali pa kuona wanaume wote ni maadui au wanawake wote ni maadui,
hapana inuka tena Muombe Mungu huko upande wako atakusaidia, kwa kuwa
anakupenda sana.
Zingatia
mambo haya:
Mathayo
7:7 “Ombeni nanyi mtapewa; Tafuteni
nanyi mtaona; Bisheni nanyi mtafunguliwa”
“Ombeni nanyi mtapewa”
Hii ni hatua ya kwanza, anza kwa kumuomba Mungu
akupe mke mwema, mume mwema, mtangulize Mungu katika jamba hii, usimwendee
mungu ukiwa tayari una majibu
“Tafuteni nanyi mtaona”
Wengi wameishia kwenye hatua ya kwanza ya kuomba
wakaacha kutafuta, Baada ya kumpelekea hoja yako Mungu unataka mwenzi wa namna
gani, tafuta ni hatua ya pili.
“Bisheni nanyi mtafunguiwa”
Sasa
wengi wao hatua hii wanaiogopa ya kubisha hodi (Uthubutu) baada ya kuomba
Mungu, ukatafuta kinacho fuata ni kuthubutu, Mwambie mimi nie……… nataka……… mwa 2:23 “Adamu akasema, sasa huyu ni mfupa
katika mifupa yangu na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamk, kwa
maana ametwaliwa katika mwanaume”
Usiache kufuatilia:
0 comments:
Post a Comment