Wednesday, 27 December 2017


Bwana Yesu asifiwe,

Yako mambo kadha ambayo ukiyachunguza unaweza kuutambua wito wako kwa haraka zaidi na kukuondoa kwenye sitofahamu ya wito wako. Watu wengi kanisani wanamtumikia Mungu chini ya viwango si kwasababu hawampendi Mungu ila kwasababu hawajajua wito wao kila kona utawakuta sikwamba wao ni kimbele mbele ila hawajajua ni eneo gani ambalo Mungu amewaitia ili wakae katika eneo hilo na kufanya katika viwango

Mf. Kuimba hupo, kufundisha hupo, kuhubiri yupo, kuonya yupo, kuchunga, kufariji yupo nk na vyote anafanya juu juu tu, si katika kiwango ambacho Mungu anachotaka, kwasababu hawajajikita kwenye wito wao.

Fuatilia zaidi ujifunze kwa kina namna ya kuujua wito wako kibiblia, kama ifuatavyo;-
  1. Amani na Furaha ya moyoni
  2. Kupenda na Kuridhika
  3. Kutumia Muda Zaidi
  4. Uwezo mkubwa ktk hilo
  5. Matokeo Mazuri
  6. Baraka na Mafanikio
  7. Ushuhuda mzuri wa wengine

Unaujuaje wito wako?.



1 Amani na Furaha ya moyoni
Isaya 55:12,
“Maana mtatoka kwa furaha, mtaongozwa kwa amani” katika kuujua wito wako jiulize maswali hay, Je! Hili ninalolifanya ndani yake ninapata furaha na amani au najilazimisha tu,
Filipi 4:4-7,
“Furahini katika Bwana siku zote; tena nasema furahini.  Na Amani ya Mungu ipitayo akili zote itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu” katika mistali hii inaweza kukusaidia kujipima katika kila huduma unayoifanya je ni yako au ya mtu mwingine.
Unapotumika katika eneo hilo ndandi ya moyo wako kunajawa na furaha na Amani au unakuwa kawaida tu au unafanya kwa kusukumwa.
Kolosai 3:15
“Na Amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu; ndiyo mliyoitiwa katika mwili mmoja; tena iweni watu wa shukrani” Je amani ya kristo ndani yako inaamua nini, Au jambo gani unapolifanya unasikia Amani katika Mungu.
Zab 16:11,
Kwenye wito wako lazima utapata furaha tele na mema


2.      Kupenda na Kuridhika
Kut 33:12-14
Mungu anamwambia Musa “Uso wangu utakwenda pamoja nawe, nami nitakupa raha” kwamba katika wito huo hutanitumikia tu bali nitakupa raha. Moyo wako hautapungukiwa katika kufurahia wito wako, huta kaa ujute.
 Math 11:29-30
“Jitieni nira yangu” kuambatana na Yesu/Ukikaa katika wito wako “Nanyi mtapata raha nafsini mwenu” utapata raha. Ukiona unafanya huduma Fulani na katika hali ya kuifanyia kazi moyo wako haupokei kitu kwa Mungu jiulize Je! Huu ni wito wangu kweli au ni eneo linguine.


3.      Bajeti ya Muda zaidi
Katika eneo ambalo ni wito wako utaona jinsi unavyo jishughulisha na jambo hilo kwa muda mrefu kuloko mambo mengine.
Mf. Mkulima utamjua kwa jinsi anavyojishughulisha sana na kilimo, mfugaji atajihusisha sana na ufugaji kuliko kitu kingine, hilo tu ni kiashiria cha kuonesha kuwa mtu huyo ni wa namna gani
Kut 33:7-11,
Musa sikuzote alikuwa anabeba hema la kukutania na kuhudumu watu wa Mungu, kwasababu huo ndio ulikuwa wito wake. Mungu alimuita katika eneo hilo.
Je! Wewe ni utumishi upi unaokuchukua muda mwingi?


4.      Uwezo mkubwa wa Kazi hiyo
Mtu ambaye kaitwa katika eneo Fulani utaona uwezo mkubwa alionao katika kufanya jambo hilo.
Kutoka 31:1-5,
Mungu anamwambia Musa “ nimemwita Bezaleli, name nimemjaza Roho ya Mungu, katika hekima na maarifa, na ujuzi na mambo ya kila aina. Ili abuni kazi za ustadi……….” Bezeleli alikuwa na uwezo mkubwa katika hekima, maarifa na ujuzi vitu vilivyo onesha dhahili wito wake kwa Mungu
Matendo 6:7-10.
Stefano alikuwa na uwezo mkubwa katika kufanya maajabu na ishara kubwa, hii ilionesha wazi wito wake.
Jiulize wewe una uwezo mkubwa katika kufanya wito upi? Pia inawezekana ukawa na wito zaidi ya moja sio tatizo, muhimu kila wito Mungu aliouweka ndani yako uutumikie katika viwango ambavyo vinatakiwa.
5.      Matokeo Mazuri 
Kwenye wito huo unaotumika Je! Unapata matokeo gani? Mazuri au mabaya. Pia unaweza kukapata matokeo mabaya katika wito ambao ni wako kwasababu tu yakukosa maandalizi, kuishi maisha yasiyompendeza mungu nk.
Yohana 5:36,
Kazi unazozifanya na matokeo yake ndizo zikushuhudie kuwa wewe umeitiwa katika eneo gani
Marko 16:15-20,
“Na ishara hizi zitafuatana na…..” Matokeo ya mazuri ya kazi uliyoifanya ni dalili tosha ya kukujulisha wito wako.
Matendo 8:4-8.


6.       Baraka na Mafanikio
Unapokanya wito wako Baraka na Mafanikio lazima vikuambate
Zaburi 1:3,
“Nae atakuwa kama mti uliopandwa; kando ya vijito vya maji, Uzaao matunda yake kwa majira yake, Wala jani lake halinyauki; na kila alitendalo litafanikiwa.”
 Mithali 10:22
“Baraka ya bwana hutajirisha, wala hachanganyi huzuni nayo” Katika eneo ambalo ni wito wako huwezi kuwa na huzuni bali utaambatana na Baraka tele katika wito huo.
Mith 17:8,
“Kipawa ni kitu cha thamani kwake yeye aliyenacho, kigeukapo hufanikiwa” kipawa ni wito wa mtu, anasema kila kigeukapo hufanikiwa”mtu akikifanyia kazi utafanikiwa, utapata mapokeo mazuri katika wito huo.


7.      Ushuhuda mzuri wa Watu wengine
Math 18:16,
“Zawadi ya mtu humpatia nafasi, humleta mbele ya wakuu” wito wa mtu unampatia mtu nafasi/kibali katika eneo la wito wake, kwasababu watu wanaona ni eneo gani ambalo wewe unafanya vizuri.
Yoh 3:1-2,
Nikodemu alimshuhudia Yesu kuwa ni nani, Alikuwa anaona kilichopo ndani ya Yesu
Mdo 6:1-8.
Mitume alichagua watu saba watakaosimama kwa ajili ya kutoa huduma kwa wahitaji kulingana na wito wao. Wito ndani mtu hauwezi kijificha labda mtu mwenyewe asitake kutumika.

Nimeeleza kwa kifupi tu vigengele kadha vitakavyo kufanya uweze kuutambua kwa haraka wito wako kwa Mungu ili usigongane na watu wengine katika wito wao. Bila kuzingatia hayo utajikuta kila siku unatumika chini ya kiwango kwasababu ya kutokaa katika eneo lako mpaka kufikia hatua ya kuona kama wokovu ni mzigo au hauna faida yoyote.

Mungu anakufundisha ili upate faida, Usiwe na utumishi usiokuwa na faida yoyote pia ujue namna ya kusimama katika wito wako

Mungu akutie nguvu katika utumishi wako


Mungu akubariki sana!

 Fuatilia zaidi masomo haya na mengine katika kitandao ya kijamii kama ifuatavyo;-
Blog:                    -        mungupendo.blobspot.com
Facebook:           -        Mungu Anakupenda
Youtube:              -        Mungu Anakupenda
Twitter:                -        Mungu Anakupenda



Thursday, 14 December 2017

Namna ya kumpata Mwenzi wa maisha angalia video hii ujifunze mambo mengi kuhusu mambo yahusuyo mahusiano.

Tuesday, 12 December 2017

Bwana Yesu asifiwe,

Wakati wa kuoa ni wakati wa ujana Mal 2:14 Biblia inasema mke wa ujana wako, hii inaonesha kibiblia wakati sahihi wa kuoa ni wakati wa ujana, hakuna wakati mwingine ambao ni sahihi sana wa kumpata mwenzi wa maisha isipokuwa ujanani.

Mtu wa kwanza kuwepo duniani ni kijana moja Adamu na mkewe Hawa ambao Mungu aliwapa maagizo ili wazae ili tuongezeke, Kabla hawajatenda dhambi Adamu anazungumza Utamwacha baba yako na mama yako utaambatana na mwenzi wako na mtakuwa mwili mmoja hata hakujawa na dhambi duniani.

Tunapozungumza suala la mahusiano ya kijana na Binti tunazungumzia suala takatifu kwasababu aliyelianzisha  wa tendo hili ni mtakatifu, ni sisi tumekuja kuingiza mambo mengi na kufanya suala hili kuharibika

Mahusiano  yanapitia hatua kadha wa kadha kama ifuatavyo:-
1.      Urafiki
Ni mahusiano ya kawaida ambayo kijana wa kiume na kijana wa kike wanaweza kuwa wanashirikiana katika mambo mbalimbali ya kijamii, kimasomo, kiuchumi hata kisiasa bila kuwa na agenda nyingine

2.      Uchumba
Ni mahusiano ya kijana wa kiume na kijana wa kike ambao wamekwisha peana ahadi ya kuoana. Katika hatua hii huwezi kumuita mchumba wako mke au mume.

Ni kipichi cha matazamio cha watu wawili wa jinsia ya kiume na jinsia ya kike kabla ya kuoana au kuna Ahadi ya kuoana, uchumba sio urafiki wala sio ndoa.

3.      Ndoa
Ni mahusiano ya kijana wa kiune na kijana wa kike ambao wamekwisha weka agano la kuishi kama mume na mke.

Kuna agano la watu wawili wa jinsia ya kiume na jinsia ya kike la kuishi pamoja kama mume na mke.

Mambo ya kuzingatia kwa kijana wa kiume kabla hujatafuta mwenzi:-

1.      Kumpokea yesu
Ukipatana na Mungu, Mungu Mungu atakusikiliza nawe utasikiliza, Ni vema kupatana na Mungu kwanza.

2.      Kufanya kazi
Usichumbie kama huna kazi, Mwa 2:8 Mungu alimuweka Adamu Edeni kwanza alime (Afanye kazi) ndipo alipo mletea mke (Hawa)Mwa 2:18 hivyo lazima ufanye kazi

3.      Kupata mwenzi
Mwa 2:18 Neno linasema “Bwana Mungu akasema,Si vema mtu huyu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana nae.”
Hata kama umewahi kukosea katika kufanya uchaguzi ikakupelekea kuumizwa bado una nafasi ya kuinuka tena Mit 24:16 “Bali mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena; Bali wasio haki hukwazwa na mabaya” Inawezeka na mpaka sasa umefikia mahali pa kuona wanaume wote ni maadui au wanawake wote ni maadui, hapana inuka tena Muombe Mungu huko upande wako atakusaidia, kwa kuwa anakupenda sana.

Zingatia mambo haya:
Mathayo 7:7  “Ombeni nanyi mtapewa; Tafuteni nanyi mtaona; Bisheni nanyi mtafunguliwa”

“Ombeni nanyi mtapewa”
Hii ni hatua ya kwanza, anza kwa kumuomba Mungu akupe mke mwema, mume mwema, mtangulize Mungu katika jamba hii, usimwendee mungu ukiwa tayari una majibu

“Tafuteni nanyi mtaona”
Wengi wameishia kwenye hatua ya kwanza ya kuomba wakaacha kutafuta, Baada ya kumpelekea hoja yako Mungu unataka mwenzi wa namna gani, tafuta ni hatua ya pili.

“Bisheni nanyi mtafunguiwa”
Sasa wengi wao hatua hii wanaiogopa ya kubisha hodi (Uthubutu) baada ya kuomba Mungu, ukatafuta kinacho fuata ni kuthubutu, Mwambie mimi nie……… nataka……… mwa 2:23 “Adamu akasema, sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamk, kwa maana ametwaliwa katika mwanaume”

Mungu akubariki sana   

Usiache kufuatilia:

Youtube       Facebook          Twitter



Monday, 11 December 2017


1.   Yesu kwetu ni rafiki, hwambiwa haja pia;
      tukiomba kwa Babaye, maombi asikiya;
       Lakini twajikosesha, twajitweka vibaya;
       kwamba tulimwomba Mungu, dua angesikia.

2.   Una dhiki na maonjo? Una mashaka pia.
  Haifai kufa moyo, dua atasikia.
          Hakuna mwingine mwema, wa kutuhurumia;
          atujua tu dhaifu; maombi asikia.


3.   Je hunayo hata nguvu, huwezi kwendelea,
  ujapodharauliwa, ujaporushwa pia.

       Watu wangekudharau, wapendao dunia,
       hukwambata mikononi, dua atasikia.
1. Ni tabibu wa karibu; tabibu wa ajabu;
na rehema za daima; ni dawa yake njema.

Imbeni, malaika, sifa za Yesu Bwana;
pweke limetukuka jina lake Yesu.
                     Hatufai kuwa hai, wala hatutumai,
                     ila yeye kweli ndiye atupumzishaye.

2. Dhambi pia na hatia ametuchukulia;
Twenendeni na amani hata kwake mbinguni.

3. Huliona tamu jina, la Yesu kristo Bwana,
yuna sifa mwenye kufa asishindwe na kufa.

4. Kila mume asimame, sifa zake zivume;
Wanawake na washike kusifu jina lake.


5. Na vijana wote tena, wampendao sana,
waje kwake wawe wake kwa utumishi wake.

1.Mwokozi umeokoa, nimekuwa wako wewe,
damu imenisafisha; sifa kwa mwana kondoo.

Utukufu, Aleluya! Sifa kwa mwana kondoo!
 Damu imenisafisha, utukufu kwa Yesu!

2.Nilijitahidi sana, ila sikupata raha,
bali kwa kumtegemea, nilipata Baraka

3.Daima namwegemea, damu ikifanya kazi,
nikioga kwa chemchemi, itokayo mwokozi.

4.Sasa ninewekwa wakfu; Nitaishi kwako wewe:
Fahari nashuhudia, ya wokovu wa bure.

5.Nasimama kwake Yesu, ameponya roho yangu:
ameniondoa dhambi, anifanye mzima.

6.Nilikuwa kifungoni, niliteswa na dhambi,
nilifungwa minyororo, Yesu akanifungua.

7.Sifa, ameninunua! Sifa, nguvu za mwokozi!
Sifa, Bwana huhifadhi! Sifa zake milele.

Thursday, 7 December 2017

Monday, 4 December 2017

1. Mungu ni pendo apenda watu,Mungu ni pendo anipenda

      Sikilizeni furaha yangu,
       Mungu ni pendo, anipenda
2. Nilipotea katika dhambi,
nikawa mtumwa wa shetani
3. Akaja Yesu kuniokoa,
yeye kanipa kuwa huru
4. Sababu hii namtumikia,
namsifu yeye siku zote.

Followers

Social Networks

Popular Posts

Blog Archive